Baraza La Vijana Wilaya Ya Mjini.

Baraza La Vijana Wilaya Ya Mjini. Zanzibar youth council is semi autonomous co-operate organization which established by the aim of having unified voices so advocate,lobby youth development

Ni chombo kinacholusanya saut za vijana na kusaidia katika maendeleo yao na taifa kwa ujumla.

15/07/2021
15/07/2021
13/06/2018

Habari za asubuhi kupitia maazimio ya mkutano kupitia mamalaka niliyonayo k**a Mwenyekiti,kwa niaba ya baraza la ya Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini.

Napenda kuitangaza ramsi k**ati itakayofuatilia madeni yote tunayoyadai kwa watu mbalimbali.Kama ifuatavyo
1.Fransisca Camilius Clement (Mwenyekiti wa Kamati).
2.M***a Kassim M***a (Katibu wa Kamati)
3. Ali Rajab Issa (Naibu Katibu)
4.Abdulatif Ali Yasin (Mjumbe)
5. Suleiman Ali Khamis(Mjumbe)
6.Khadija Abdulrahman Mwinshaa (Mjumbe)
7. Mode Khelef Mohd (Mjumbe)
8.Yussuf Kheri Ali (Mjumbe)

Naomba kuwasilisha.

Imetolewa tarehe 13 Juni 2018.

By Mwenyekiti Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini.

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini akifungua mafunzo ya siku tatu hapo ukumbi wa sebleni yalioandaliwa na Bi...
29/04/2018

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini akifungua mafunzo ya siku tatu hapo ukumbi wa sebleni yalioandaliwa na Bi Abla Mohd Baraka kupitia Kampeni yake ya "Mwanamke Chakarika" hapo siku ya Ijumaa.

Mh naibu waziri wa vijana Mh Lulu Msham akihojiwa na wanahabari vijana baada ya kuwatembele wakiwa katika mafunzo akifua...
28/03/2018

Mh naibu waziri wa vijana Mh Lulu Msham akihojiwa na wanahabari vijana baada ya kuwatembele wakiwa katika mafunzo akifuatana na Rais wa wasanii Zanzibar.

Mafunzo hayo yaliwashirikisha vijana kutoka mabaraza ya vijana wilaya ya mjini Unguja.

Wakishirikiana na taasisi kutoka Mwanza inayoitwa Mwanza Youth and Children Network.

Tukiwa katika picha ya pamoja kati ya viongozi wa Baraza la Vijana.Wilaya ya Mjini na Baraza la vijana Zanzibar hapo jan...
28/03/2018

Tukiwa katika picha ya pamoja kati ya viongozi wa Baraza la Vijana.Wilaya ya Mjini na Baraza la vijana Zanzibar hapo jana baada ya kufunga mafunzo ya wanahabari vijana.

Baraza la vijana wilaya ya mjini,wamefunga mafunzo ya wanahabari vijana na wanahabri hao kufungua information center amb...
28/03/2018

Baraza la vijana wilaya ya mjini,wamefunga mafunzo ya wanahabari vijana na wanahabri hao kufungua information center ambayo itatumiaka na wanahabi hao ili kuhakikisha elimu na vipaji vyao havipotei.

Mafunzo hayo yalifungwa na Mh naibu mkurugenzi wa ZBC Bi Nasra Mohd hapo raha leo studio.

Hatimae Wajerumani wafika katika kuangalia namna gani wanaweza kuitengeneza Botanic Garden inayomilikiwa na Baraza la Vi...
13/03/2018

Hatimae Wajerumani wafika katika kuangalia namna gani wanaweza kuitengeneza Botanic Garden inayomilikiwa na Baraza la Vijana Shehia ya Kilimani iliyopo Wilaya ya Mjini Unguja.

13/03/2018
Baraza la vijana wilaya mjini lashiriki katika bunge la vijana Zanzibar kuelekea maadhimisho ya siku ya jumuiya ya madol...
13/03/2018

Baraza la vijana wilaya mjini lashiriki katika bunge la vijana Zanzibar kuelekea maadhimisho ya siku ya jumuiya ya madola.

Baadhi ya viongozi wa Baraza la Vijana Zanzibar wakiwa katika picha ya pamoja.

Baraza la vijana wilaya ya mjini lapatiwa mafunzo juu ya fursa zilizopo katika jumuiya ya Afrika Mashariki .Mafunzo hayo...
05/03/2018

Baraza la vijana wilaya ya mjini lapatiwa mafunzo juu ya fursa zilizopo katika jumuiya ya Afrika Mashariki .

Mafunzo hayo yalifanyika.leo aaubuhi hapo ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani.

Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mjini wakishirikiana na Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini katika kuebdeleza program ya usafi h...
04/03/2018

Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mjini wakishirikiana na Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini katika kuebdeleza program ya usafi huko shehia ya Kwa Wazee Sebleni Zanzibar.

Baraza la vijana-wilaya ya mjini, ikishirikiana na OFISI YA MKUU WA WILAYA YA MJINI na wadau wa maendeleo ya vijana, wan...
02/10/2017

Baraza la vijana-wilaya ya mjini, ikishirikiana na OFISI YA MKUU WA WILAYA YA MJINI na wadau wa maendeleo ya vijana, wanakuletea MDAHALO WA WAZI wenye mada "JE! RASILIMALI NA UCHUMI TULIONAO UNAWEZA KUTUFIKISHA KATIKA TANZANIA YA VIAWANDA" Nyote mnakaribishwa, jaza fomu kwenye link ifuatayo kwa uthibitisho wa ushiriki/uchangiaji wako.

https://docs.google.com/forms/d/e/1FAIpQLScb0wlSLCxBACPZFDAU2Sbhfxr3MaTMnMSRUi6mJSckeflrcA/viewform

Ahsante.

Imetolewa na;
TARIQ A KHAMIS
/BARAZA LA VIJANA
WILAYA YA MJINI.
+255 772 704 400

Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini katika kuadhimisha kilele cha siku ya vijana duniani imeweza kushiriki kongamano lililo...
13/08/2017

Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini katika kuadhimisha kilele cha siku ya vijana duniani imeweza kushiriki kongamano lililoandaliwa Na idara ya vijana,Zafayco,na pia mechi ya kombe la mbuzi iliuokua imeandaliwa Na jumuiya ya Mydo ikiwa na lengo kuhamasisha amani Na upendo katika jamii Mgeni rasmi akiwa Mh mwakilishi wa jimbo la Chaani Mh Nadir,ujenzi wa taifa katka kuunga mkono jitihada zinazoendelea kufanywa na Mkuu wa Mkoa wa mjin Magharib Mh Ayoub Mahmoud kupitia kampeni yake ya mm na wewe.

08/08/2017

RIPOTI YA MWAKA MMOJA TOKA KUANZISHWA BARAZA LA VIJANA LA WILAYA YA MJINI.

UTANGULIZI;
Baraza la Vijana ni Taasisi yenye kujitegemea iliyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria nambari 16/2013 iliyopitishwa na kutiwa saini na Mh. rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohammed Shein
Baraza la Vijana ni chimbuko la Sera ya maendeleo ya Vijana ambayo iliandikwa na wadau baada ya kuona uwakilishi wa Vijana katika masuala yanayowahusu Vijana uzingatiaji na ushiriki ni mdogo.
Hivyo basi hadi mwaka 2013 ilianzishwa rasmi sheria ya Mabaraza ya Vijana na kupitishwa ndani ya Baraza la Wawakilishi chini ya Uongozi wa Raisi wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk: Ali Mohammed Shein ambaye aliatia saini Sheria ya uwanzishwaji wa Mabaraza hayo Sheria No 16 ya mwaka 2013
Mabaraza yameanzishwa kwa malengo yafuatayo:-
• Kuwajenga viajna kutambua utaifa wao ili kuongeza uzalendo na imani ya kuipenda nchi yao.
• Kuwa kiungo wakilishi na jukwaa la kutetea na kulinda maslahi ya vijana nchini.
• Kkushajihisha kujengewa uwezo kwa vijana ili kuwa wajenzi imara wa taifa na jamii .
• Kuwakilisha maslahi ndani ya vijana na nje ya nchi
• Kuongeza ushiriki wa vijana katika ngazi mbalimbali za maamuzi na katika ngazi za kiongozi.
Mchakato wa uhamasishaji ulianza mwaka 2014 ambapo takribani ya vijana elfu 2000 walifikiwa katika shehia zote za wilaya mjini, hatimae kuanza hatua nyengine kwa ajili ya uchaguzi wa viongozi wa mabaraza kwa ngazi mbali mbali ngazi ya shehia na Wilaya.

Katika ngazi ya Shehia nafasi zilizogombaniwa ni:-
• Mwenyekiti
• Makamo Mwenyekiti
• Katibu
• Wajumbe 9 wa k**ati tendaji
Katika ngazi ya Wilaya nafasi zilizogombaniwa ni:-
• Mwenyekiti
• Makamo mwenyekiti
• Wajumbe 7 wa k**ati tendaji
Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini lina jumla ya wajumbe 55 ambao ni wenyeviti wa mabaraza shehia
Baraza la vijana wilaya ya mjini linaundwa na wanachama wapatao 1860 wavulana 740 na wasichana 1120 kutoka shehia 55 zilizomo ndani ya wilaya ya mjini.
1. MAFANIKIO
Miongoni mwa mafanikio hayo ni k**a ifuatavyo:-
Kupatiwa kwa mafunzo kwa wanachama wa baraza
• Uongozi – uendeshaji wa Baraza na namna kuendeleza Taasisi, jumla ya Vijana wapatao 900 walipatiwa Mafunzo ya Uongo ambayo yalidhainiwa na Eqwips Hubs
• Ujasiriamali- Utengenezaji wa Sabuni,Shampoo,Taiz , Vijana 72 walipatiwa Mafunzo. ambapo jumla ya Vijana kumi na tano ( 15) wasichana walipatiwa Mafunzo jinsi ya kutengeneza mbolea za asili, kutengeneza mizinga ya Nyuki, kutengeneza dawa za asili bila ya kutumia kemikali, jinsi ya kutayarisha shamba na mbinu mbali mbali za kujikwamua kiuchumi.
• Kilimo :Mafunzo haya yalifanyika chini ya udhamini mradi wa Fursa kijani na Milele foundation, ambayo katika mafunzo hayo vijana watano wameweza kupatiwa Ajira.
• Sanaa na Ubunifu
• Uzalendo
• Kupiga kura
• Sheria

• Stadi za maisha takriban 100 walipatiwa Elimu za stadi za maisha ili kuweza kujitambua na kuepukana na changamoto za kundi rika ambazo hukabiliana nazo kila siku.
• Ukomavu wa kifedha (Eqwip hub)
• Utalii Jumla ya Vijana 10 waliweza kupatiwa Mafunzo ya Hotelia ambayo Mafunzo hayo yaliandaliwa na ILO na ZITOD kwa kushirikiana na Wizara ya kazi Zanzibar kwa lengo la kuinua fursa za vijana wa Zanzibar.

FURSA ZA AJIRA
• Kuajiriwa na vikosi mbali mbali – JKU na vikosi vyengine.
• Mahotelini
• Kujiajiri
• Takriban Vijana 43 wameajiriwa na waliojiri kupitia fursa mbali mbali ni Vijana 15.
• Uandishi wa miradi
• Mradi wa Chaki
• Jiwe Jeusi
• Uwezeshaji kiuchumi
• Taka ngumu na laini ( recycling process)
• Ufugaji wa kuku
• Kukuzamichezo na utamaduni
• Elimu ya lugha ya kiingereza
• Utumiaji sahihi wa rasilimali

2. USHIRIKI NA USHIRIKISHWAJI
Katika suala la ushiriki na ushirikishwaji limeongezeka kwa takriban asilimia 60% kitu ambacho kimeweza kufikia malengo ya uanzishwaji wa mabaraza ya Vijana .
Hili limeonekana katika kipindi cha mwaka mmoja kupitia Ushiriki na Ushirikishwaji wa Vijana kupitia Serikali na Sekta binafsi k**a ifuatavyo:-
• Utungaji wa Sera k**a ya Vijana,Uchumi na Afya
• Uandaaji wa mipango kazi na mikakati k**a vile wa tume ya Ukimwai Zanzibar
• Kongamano za kiutamaduni k**a vile Zanzibar International Film Festival (ZIFF)
• Udhibiti juu ya mipango ya Madawa ya kulevya.
• Kampeni za kusaidia Jamii k**a Mimi Na Wewe na Kijana paza sauti.
• Uandaaji wa Nakala na Vipeperushi mbali mbali vinavyohusu Vijana
• Ushiriki wa siku za maadhimisho mbali mbali za Kimataifa k**a vile siku ya mtoto Njiti ,mabaharia,madawa ya kulevya,ukimwi nk.
Baraza la Vijan wilaya ya Mjini limesaidia kuhamasisha Vijana katika kuzitambua na kuzifikia fursa zinazo walenga moja kwa moja mfano bahari, bahari ikitumiwa vizuri inaweza ikawa ni sehemu kubwa ya kuondoa tatizo la Ajira kwa Vijana wetu, pia taka ngumu, ambazo taka hizo baada ya kuzisanifu kutoka katika uhalisia wake na kuweza kukifanya kitu kipya ambacho kinaweza kikatumika katika maisha ya kiujumla, Ardhi katika matumizi ya kilimo k**a tujuavyo kwamba ardhi ndio uti wa mgongo wa taifa letu, hivyo Vijana wetu wakiitumia vidhuri ardhi hii kwa kilimo cha kisasa itawatoa katika moja na kuwapeleka hatua nyengine
3. MAHUSIANO NA TAASISI MBALIMBALI
EQWIPHUB ZAFAYCO
MICHAEL JOHNSON MYDO
UNFPA VSO
SAMBA FOUNDATION ZURA
TASAF JABAL NOR
ZACA ZAC
CYD ZLSC
ZYF ZAYEDESA
SYPC MELISHA

SERIKALI
• Ofisi ya Makamo wa pili wa Rais
• Wizzara inayohusiana na masuala ya vijana
• Wizara ya habari
• Wizara ya afya
• Wizara tawala za mikoa
• Ofisi ya mkuu wa mkoa
• Ofisi ya mkuu wa wilaya
4. CHANGAMOTO.
Licha ya Mafanikio hayo yote kipindi cha mwaka mmoja kilikua ni kipindi kikubwa cha kujifunza na kujipanga imara katika kuhakikisha dhana nzima ya Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini yanafikiwa sambamba na malengo ya uanzishwaji wa baraza la vijana Zanzibar.
Hivyo baraza la vijana lilikumbana na miongoni mwa changamoto ambazo zinahitaji kufanyiwa kazi kwa pamoja na kushirikiana na baraza la wilaya ya mjini’
Miongoni mwa changamoto hizo ni k**a ifuatavyo:
• Kutojuulikana lengo kuu la Baraza la Vijana
• Kutoungwa mkono na baadhi ya taasisi za kiserikali na binafsi
• Dhana nzima ya kujitolea na utetezi.
• Kutokuwepo kwa bahshish kwa viongozi wa Mabaraza
• Uhaba wa vitendea kazi k**a kamera ,laptop,desktop na projector
• Ukosekanaji wa miundo mbinu ya kutendea kazi
• Uelewa mdogo juu ya dhana nzima ya uongozi
• Uwepo wa muhali kwa viongozi wa juu katika kuchukua hatua juu ya kulinda haki za vijana na kuskilzwa k**a sheria inavyoelekeza.

5. MAPENDEKEZO
• Serikali kuongeza mbinu za ufanisi katika kuhakikisha vijana wanaendelea kupewa kipaumbele nchini kupitia mabaraza hususan fursa zinazowahusu vijana.
• Serikali kuondoa sheria au kuzirekebisha ili kuhakikisha maslahi ya vijana yanafikiwa k**a malengo ya uanzishwaji yalivyo. Mfano udhalishaji na unyanyasaji,baraza la vijana baadhi ya vifungu nk.
• Sekta binafsi kuwapa vipaumbele vijana kupitia Baraza la vijana wilaya mjini juu ya fursa zilizopo.
• Vijana kujiunga na kuibeba dhana ya kujitolea k**a sehemu ya kujipatia uzoefu na kuongeza network na wadau mbalimbali ili kufikia malengo yao .

HITIMISHO
Shukrani zetu za dhati kabisa zimuendee mh Raisi wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baaza la Mapinduzi Dk. Ali Mohammed Shein kwa kutuletea chombo ambacho kina mnasaba wa kuunganisha sauti za vijana ili kujitetea na kusaidia taifa katika kutatua changamoto zao na taifa kwa ujumla.
Pili kuishukuru wizara ianyohusiana na masuala ya vijana,
Ofisi ya mkuu wa mkoa wa mjini mgahribi kwa mchango mkubwa na kuwa sambamba na vijana bega kwa bega.
Ofisi ya mkuu wa wilaya ambayo imekua bega kwa bega kushirikiana nasi kwa kila jambo tunalifanya basi mkono wa fisi hii uko ,hongera zifikie hususani kwa mkuu wa wilaya ya mjini.
Bila ya kuwasahu wadau mbalimbali k**a vile eqwiphub ,mydo,Zanzibar youth council na wadau mbalimbali ambao wengine wapo nasi hapa hii leo.
MUELEKEO WABAADAE
• Baraza la Vijana wilaya ya Mjini kua ni Chombo cha mabadiliko chanya katika jamii
• Kuwa ni sehemu ya utetezi wa masuala ya vijana nchini
• Kuongeza wanachama ili kuwa na sauti yenye nguvu nay a kusikika ili kufikia malengo yake.

Baraza la Vijana Wilaya ya mjini katika kuadhmisha mwaka mmoja likiwa katika ukumbi wa Baraza la wawakiliahi la zamani k...
08/08/2017

Baraza la Vijana Wilaya ya mjini katika kuadhmisha mwaka mmoja likiwa katika ukumbi wa Baraza la wawakiliahi la zamani katika utoaji wa ripoti ya mwaka Mmoja ambapo mgeni rasmi alikua ni Waziri wa habari,utalii,utamaduni,sanaa na michezo sambamba na kutoa vyeti mbalimbali kwa Vijana ambao walifanya juhudi katika uhamaaishaji wa uundwaji wa mabaraza Wilaya ya mjini.

By Mwenyekiti k**ati ya Mawasiliano Baraza La Vijana Wilaya ya Mjini.

05/08/2017
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mheshimiwa Ayoub Mohamed Mahmoud akiwa Sambamba na Mkuu wa wilaya ya Mjini Bi. Marina Jo...
03/08/2017

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mheshimiwa Ayoub Mohamed Mahmoud akiwa Sambamba na Mkuu wa wilaya ya Mjini Bi. Marina Joel Thomas mara baada ya kupokea matembezi yaliyoandaliwa na Baraza la Vijana Wilaya ya Mjini katika kusheherekea kutimiza mwaka mmoja pamoja na kuelekea maadhimisho ya siku ya vijana duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni "VIJANA NI WAJENZI WA AMANI". Matembezi hayo yalianzia Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya mjini mpaka Mapinduzi square hapo Kisonge ambapo palifuatiwa na zoezi la uchangiaji damu. Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi pamoja na Mkuu wa wilaya ya mjini pia walishiriki matembezi hayo katika kuwaunga mkono vijana.
Na,
Mwenyekiti Kamati ya Mawasiliano.
Baraza la vijana wilaya ya mjini.

Address

Zanzibar City
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 15:00
Tuesday 09:00 - 15:00
Wednesday 09:00 - 15:00
Thursday 09:00 - 15:00
Friday 09:00 - 15:00

Telephone

+255657622034

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Baraza La Vijana Wilaya Ya Mjini. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Baraza La Vijana Wilaya Ya Mjini.:

Share