09/06/2023
✍️ Anaandika Feisal Salum
Ndugu zangu Watanzania;
Kwanza namshukuru Allah kwa kila jambo, kwa utulivu wa nafsi na namna alivyonijalia hadi muda huu nikiwa mchezaji wa Azam Fc.
Namshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia kwa namna ya kipekee na namna anavyofuatilia michezo na kutulea sisi watoto wake. Binafsi sina la kumlipa zaidi ya kuifia jezi ya Timu ya Taifa ya Tanzania.
Nawashukuru Watanzania wote kwa mapenzi yao kwangu, nawashukuru Mashabiki wa Yanga na uongozi kwa miaka yote tulokua pamoja, haikua rahisi mimi kuondoka.
Kipekee niwashukuru wachezaji wote nilocheza na Yanga na kufurahia michezo mingi ya ushindi na kumbukumbu nyingi pamoja. Hatukuwa tu wachezaji wa timu moja bali familia.
Niwashukuru Azam Fc kwa kuona nafaa kucheza timu hii na nawaahidi ubora na jasho la kweli kutafuta mafanikio. Kwangu mimi hii ni klabu kubwa yenye hadhi ya mimi kuichezea.
Maisha mapya yameanza, tuvae jezi namba 6 ya na tujae kwenye michezo yetu, nyakati mpya zimeanza.
✍️