12/05/2026
Wakala wa FIFA kutoka nchini Uganda, Ronnie Santos Mwine Fred ameripoti kuwa, Maskauti wa vigogo wa 🇹🇷Uturuki Fenerbahçe SK wamekuwa 🇹🇿Tanzania kwa siku ya 4 sasa, na sababu pekee ni nyota kijana wa timu ya taifa ya 🇺🇬Uganda "The Cranes" Allan Okello!
Na Watamfuatilia tena katika mchezo ujao dhidi ya Dodoma Jiji.
Katika mechi ya kwanza waliyomtazama, alifunga mabao 2 na kutoa assist 1 dhidi ya Coastal Union
Young Africans S.C. wanatajwa kuhitaji takribani dola milioni 3 (Tsh 7.8B) kwa nyota huyo wa timu ya taifa ya Uganda, The Cranes.