Amputee Football for Africa

Amputee Football for Africa Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Amputee Football for Africa, Sports Event, Tanzania National Stadium, Dar es Salaam.

27/05/2024

UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI CECAAF IMEANGUKA - MASHINDANO YA AFRIKA

Ni takribani miaka miwili nyuma Ukanda wa Afrika mashariki ulikuwa ni ukanda tishio katika mchezo wa Soka la walemavu katika Bara la Afrika na Dunia kwa ujumla. Ukanda huo ambao umesheheni vigogo wa mchezo huu barani Afrika wakiongozwa na Tanzania, Kenya, Uganda na Rwanda waliweza kiteka hisia za mashabiki na serikali zao kwa kufanya vizuri kwenye mashindano mbalimbali ya kimataifa.

Takwimu zinaonesha kwamba Mashindano ya mwisho ya Afrika yaliyofanywa na moja ya nchi za ukanda huo (Tanzania) chini ya udhamini wa Rais wa nchi Mh. Samia Suluhu Hassan kwa zaidi ya Dola 250,000 = Tsh. Million 600+ ya mwaka 2021, Tanzania ilishika nafasi ya 4 kwa ubora Afrika, Kenya nafasi ya 6 kwa ubora huku Uganda ikishika nafasi ya 11 kati ya nafasi 11 za afrika. Ubora wa Tanzania ulifanya Tembo Warriors ikafuzu kwenda Kombe la Dunia katia ya 4 bora za Afrika.

Mwaka huu 2024, Mashindano ya Afrika yamefanyika tena nchini Misri na nchi za Afrika mashariki zimewakilishwa na Tanzania, Kenya, Uganda na Burundi. Mashindano ya mwaka huu yalikuwa na nafasi 7 za kufuzu kwenda kombe la Dunia mwaka 2026. Mpaka sasa nchi za Afrika Mashariki zimepata matokeo ya kuporomoka kwa kasi kubwa katika viwango vya Afrika, Tanzania ikishika nafasi ya 8 kutoka 4, Kenya ikishika nafasi ya 11 ktoka 6, Uganda akiendelwa kushikilia nafasi yake ya 10 na mgeni Burundi akishika nafasi ya mwisho ya 12. K**a ni kushika Daraja basi nchi za afrika mashariki 3 zinazoshika nafasi za mwisho zingeshuka daraja.

Jambo la kusikitisha zaidi ni nchi hizi kushindwa kufuzu kwenda kombe la dunia katika nafasi 7zilizotolewa wa Afrika, Tanzania iliyokuwa inategemewa katika ukanda huu imeshindwa kufuzu kwa wageni wa mashindano haya k**a vile Moroco, Algeria na Misri ambao wanashikiri kwa mara ya kwanza au mara ya pili. Tanzania ambayo imeshiriki mashindano haya kwa mara ya tatu na kugombea nafasi ya kufuzu kwa mara ya pili imeambulia patupu k**a ilivyo kwa majirani zake. Katika mechi tano alizo cheza Tembo Warriors, ameshinda mechi moja dhidi ya Sierra Leone na kupoteza mechi zingine zote (4). Hili pigo kubwa sana kwa ukanda wetu hasa ukizingatia ukanda huu umetoa Katibu Mkuu wa shirikisho Afrika Ndg. Peter Oloo (Kenya), mwenyekiti wa uchaguzi Afrika Ndg. Kitimbo Lawrence (Uganda) na Mgombea wa Uraisi wa Afrika katika uchaguzi uliopita Ndg. Peter Sarungi (Tanzania).

Natoa pole kwa vijana wetu walio pambana kwa jasho na damu ingawa wameshindwa kufikia malengo kutokana na sababu mbalimbali hasa za usimamizi, uongozi na wa mikakati katika kuchagiza mafanikio yao. Rudini nyumbani tujipange kwa miaka mingine, 2030 sio mbali tunaweza kujisahihisha na kurudi kwenye kiwango chetu.
Nitoe rai kwa wasimamizi na viongozi kupitia maneno machache, KARMA IS REAL.





Peter Leonard Sarungi

MIAKA 30's+ YA UZOEFUYatosha kuwa na Hekima»»Na Next SpeakerMiaka ya ujana inaanza 25 hadi 45, takwimu zinaonesha kuwa 7...
06/12/2023

MIAKA 30's+ YA UZOEFU
Yatosha kuwa na Hekima»»

Na Next Speaker

Miaka ya ujana inaanza 25 hadi 45, takwimu zinaonesha kuwa 75% ya watu Africa ni vijana, kwa Tanzania ni 65% ya watu ni vijana. Niliwahi kusema kuwa ujana ndio umri pekee wenye kuandika na kufuta pale unapokosea.

Binafsi bado nipo kwenye umri wa ujana na leo nimetimiza miaka kadhaa inayovuka zaidi ya nusu ya miaka ya ujana. Namshukuru Mungu kwa kunilinda na kunitetea kwa kipindi chote hicho nikipita kwenye majaribu mbalimbambli na misukosuko. Namshukuru pia Mungu kwa mafanikio mbalimbali niliyoyapa katika kutumikia umri wa ujana. Moja ya mafanikio niliyoyapata ni kuhudumu kwenye fani mbalimbali za maisha kwa mafanikio makubwa.

Watu wengi wananifahamu kwa fani tofauti tofauti nilizokutana nao.

Kuna wanao nifahamu k**a:
Dreva wa bajaji
Derva wa Tax
Mfugaji wa kuku
Mwalimu wa sekondari na chuo
Mwasibu
Mwana siasa
Mwana harakati
Kiongozi
Mjasiliamali
Mwana michezo

Lakini pia mimi ni Mume na Baba wa watoto kadhaa. Kuna wanao nifahamu kwa ujasiri, uthubutu, misimamo, ushauri, ukorofi, uvumilivu, huruma, uwajibikaji na kujenga hoja.

Haya yote niliyopata kuyafanya maeneo mbalimbali na watu mbalimbali yamenipa elimu nzuri ya kukuza hekima na busara.

Uzoefu mkubwa niliopata ni juu ya nguvu ya maneno yanayotoka kinywani mwangu. Maneno yangu ni silaha tosha inayoweza kupambana na adui yoyote na hapa ndipo nilipojifunza kuwa na hekima na busara ya kusema kitu gani, kwa nani, mahala gani na kwa wakati gani.

Nawashukuru wote mlionitakia heri ya siku ya kuzaliwa kwangu. Mungu awabariki sana kwa kuendelea kuwa karibu na mimi

Asanteni

The Next Speaker
Peter Sarungi Jr.

MIAKA 30's+ YA UZOEFUYatosha kuwa na Hekima»»Na Next SpeakerMiaka ya ujana inaanza 25 hadi 45, takwimu zinaonesha kuwa 7...
06/12/2023

MIAKA 30's+ YA UZOEFU
Yatosha kuwa na Hekima»»

Na Next Speaker

Miaka ya ujana inaanza 25 hadi 45, takwimu zinaonesha kuwa 75% ya watu Africa ni vijana, kwa Tanzania ni 65% ya watu ni vijana. Niliwahi kusema kuwa ujana ndio umri pekee wenye kuandika na kufuta pale unapokosea.

Binafsi bado nipo kwenye umri wa ujana na leo nimetimiza miaka kadhaa inayovuka zaidi ya nusu ya miaka ya ujana. Namshukuru Mungu kwa kunilinda na kunitetea kwa kipindi chote hicho nikipita kwenye majaribu mbalimbambli na misukosuko. Namshukuru pia Mungu kwa mafanikio mbalimbali niliyoyapa katika kutumikia umri wa ujana. Moja ya mafanikio niliyoyapata ni kuhudumu kwenye fani mbalimbali za maisha kwa mafanikio makubwa.

Watu wengi wananifahamu kwa fani tofauti tofauti nilizokutana nao.

Kuna wanao nifahamu k**a:
Dreva wa bajaji
Derva wa Tax
Mfugaji wa kuku
Mwalimu wa sekondari na chuo
Mwasibu
Mwana siasa
Mwana harakati
Kiongozi
Mjasiliamali
Mwana michezo

Lakini pia mimi ni Mume na Baba wa watoto kadhaa. Kuna wanao nifahamu kwa ujasiri, uthubutu, misimamo, ushauri, ukorofi, uvumilivu, huruma, uwajibikaji na kujenga hoja.

Haya yote niliyopata kuyafanya maeneo mbalimbali na watu mbalimbali yamenipa elimu nzuri ya kukuza hekima na busara.

Uzoefu mkubwa niliopata ni juu ya nguvu ya maneno yanayotoka kinywani mwangu. Maneno yangu ni silaha tosha inayoweza kupambana na adui yoyote na hapa ndipo nilipojifunza kuwa na hekima na busara ya kusema kitu gani, kwa nani, mahala gani na kwa wakati gani.

Nawashukuru wote mlionitakia heri ya siku ya kuzaliwa kwangu. Mungu awabariki sana kwa kuendelea kuwa karibu na mimi

Asanteni

The Next Speaker
Peter Sarungi Jr.

Usiogope.Heriya mwaka mpya
27/12/2022

Usiogope.
Heriya mwaka mpya

Yes! Nipo tayari kuhesabiwa
15/08/2022

Yes! Nipo tayari kuhesabiwa

Nembo ya mashindano ya Kombe la Dunia yanayo fanyika Uturuki
15/07/2022

Nembo ya mashindano ya Kombe la Dunia yanayo fanyika Uturuki

Kujua Idadi ya watu wenye Ulemavu ni Agenda ya msingi kwa jamii husika.Tujitokeze kuhesabiwa ili tutambulike.
27/06/2022

Kujua Idadi ya watu wenye Ulemavu ni Agenda ya msingi kwa jamii husika.

Tujitokeze kuhesabiwa ili tutambulike.

A Right Magician single footed man from Ludewa- Njombe Tanzania. May God bless your talent for your prosperity and for N...
20/06/2022

A Right Magician single footed man from Ludewa- Njombe Tanzania. May God bless your talent for your prosperity and for National team Tembo Warriors.

15/04/2022
Success behind the scene is PASSION  and ABILITY
05/04/2022

Success behind the scene is PASSION and ABILITY

HONGERENI SANA WACHEZAJI WA KIMATAIFA WA TEMBO WARRIORS. Wachezaji wawili kutoka Tembo Warriors (Alfan Kiyanga na Shedra...
03/04/2022

HONGERENI SANA WACHEZAJI WA KIMATAIFA WA TEMBO WARRIORS.

Wachezaji wawili kutoka Tembo Warriors (Alfan Kiyanga na Shedrack Hebron) waliopo Uturuki kwenye klabu moja ya Sisli Yeditepe katika jiji la Istanbul wakiwa katika picha ya pamoja na kocha wa timu hiyo pamoja na wachezaji wengine wenye asili ya Africa. Timu hiyo inafundinshwa na kocha mkuu wa timu ya taifa ya Ghana aliyetwaa ubingwa wa Africa jijini Dar es Salaam mwaka 2021. Wachezaji wengine katika timu hiyo ni wale wa timu ya taifa ya Ghana.

Utafiti unaonesha kwamba wachezaji wa Tembo Warriors waliopo Uturuki kucheza mpira wa kulipwa ni faida na hazina kubwa kwa Taifa kuelekea kombe la dunia, hii inatokana na ukweli kwamba wanapata uzoefu wa kutosha wa kimataifa.
TAFF inawapongeza sana




Address

Tanzania National Stadium
Dar Es Salaam
9291

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amputee Football for Africa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Amputee Football for Africa:

Share

Category