30/10/2024
Ukisikia Yanga inavyochambuliwa na ukija kwenye uhalisia inashangaza
Kwa mfano, Yanga inayopewa tahadhari sasa, Imecheza michezo 13, ikiwa na cleansheets 12, ikifunga magoli 33 na kuruhusu bao moja tu (4-1 vs Azam). Katika michezo hiyo 13 kuna Derby tatu hapo
Yanga 1-0 Simba
Simba 0-1 Yanga
Azam 1-4 Yanga
Imagine hii timu imeshinda straight dhidi ya vigogo wa ligi hii wawili kwenye mechi tatu muhimu tena mmoja akiwa mwenyeji wa mchezo.
Ni Yanga hiyo hiyo ambayo imeshinda mechi 7 mfululuzo ya ligi bila kuruhusu bao. Wanaweza kuleta takwimu kwamba msimu uliopita tulianza vizuri. Ni kweli katika michezo 7 ya mwanzo msimu ulipita tulifunga magoli 20, msimu huu tumefunga magoli 12 magoli 8 pungufu.
Lakini msimu huo tulipoteza mchezo, 2-1 vs Ihefu, na tuliruhusu magoli matatu wakati msimu huu hatujaruhusu bao lolote. However msimu ule tulianza na mechi tano nyumbani kati ya 7 na michezo miwili ugenini (0-3 vs Geita na 2-1 vs Ihefu).
Msimu huu tumecheza mechi tatu tu nyumbani na nne ugenini. Kimsingi unapochambua lazima uzingatie matokeo kulingana na mazingira husika ya mchezo.
Licha ya ugumu wa mazingira bado Yanga ndio timu ambayo imetengeneza nafasi nyingi na kucheza soka la mipango zaidi
Kwa mfano: Yanga imepiga pasi 3049 (wastani wa pasi 435 kwa mechi) tukiwa na mechi 4 ugenini (viwanja visivyo rafiki), Makolo wana wastani wa pas 411 wakiwa na advantage ya kucheza mechi tano nyumbani.
Makolo ambao hawajadiliwi, wamecheza mechi tano nyumbani, bado tuna wazidi wastani wa pasi kwa mchezo.
Yanga leo tunaenda kucheza mechi ya tano ugenini. Yanga imecheza mechi 4 viwanja vigumu,, Bukoba, Arusha, Mbeya na Dar (ambayo hatukuwa wenyeji)
Ukirudi kwa Makolo wamecheza mechi 5 wakiwa wenyeji kwenye uwanja mzuri na bado tofauti yao ya magoli na sisi ni tofauti ya goli moja tu (Yanga 12, Makolo 13 na bado wana mchezo mmoja zaidi)
Katika mashuti 70 Yanga imepiga 40 imelenga goli, katika mashuti 95 ya Makolo mashuti 45 wamepiga nje.