29/06/2024
Nahisi kufa, mimi ni Binti wa miaka 27ðŸ˜ðŸ’”, sijaolewa ila nina mchumba wangu na sasa hivi nina ujauzito nakaribia kujifungua. Mchumba wangu yeye yuko mkoani kikazi na mimi nipo Dar ambapo nimekuja kujifungua, malengo ni mimi nijifungue ndiyo mchakato wa ndoa ufanyike kwani tushatambulishana.
Mwezi uliopita nilimuomba mchumba wangu pesa kwajaili ya kufanya Photo shoot za ujauzito wangu, kweli alinipa yeye hakuja kwakua alikua bize sana na kazi hivyo nilifanya mwenyewe.
Nilipiga picha nyingi, nilienda na rafiki yangu, nilipopiga picha sikuzipost lakini kumbe rafiki yangu alipost moja baadhi ya picha zangu. Siku mbili baadaye mchumba wangu alinipigia simu, alikua kakasirika akinilaumu kwanini nimemuaibisha, mimi sikumuelewa, alinitumia picha zangu, moja nilikua nimevaa kichupi tu huku juu sina kitu nimeshikilia matiti, nyingine nilipiga na chupi na sidiria nimeshikilai tumbo na nyingine nimekaa sijavaa kitu juu nimeshikilia matiti. Aliniambia hizo picha katumiwa na Baba yake anamuuliza huyu ndiyo mwanamke unataka kutuletea.
Jmn hizo picha nilipiga kwajaili yangu na mchumba wangu, sikupanga zitoke na sikujua k**a rafiki yangu atapost. Aliongea sana nikaomba msamaha na mchumba wangu alinielewa. Shida imekuja kwa wakwe zangu sasa, hawataki hata kunisikia, sio watu wa dini sana lakini wamemuambia mwanaume kuwa k**a ananioa basi aniolee huko huko hawataki kushiriki kwa chochote.ðŸ˜
Nimechnaganyikiwa, mchumba wangu ameniambia kanisamehe hajali ila ukiongea naye ni k**a hayuko sawa kabisa, amepunguza mawasiliano kabisa.
Alikua ni mtu wa kupiga simu kutwa zaidi ya mara 10 lakini sasa hivi anaweza kukaa hata siku mbili hapigi, ukimuuliza anadai kuwa ni kazi. Me sikupiga picha kwa nia mbaya, nilipiga tu kwaajili ya kumbukumbu, sikujua k**a zitavuja, naomba unisaidie nifanye nini ili angalau wakwe zangu wanielewe. Nampenda sana mchumba wangu lakini nashindwa kuelewa nifanye nini nisaidieni jmn naumia🥺