School KukuChoma Carnival

  • Home
  • School KukuChoma Carnival

School KukuChoma Carnival Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from School KukuChoma Carnival, Event, Dar es Salaam, .

Shule ya Sekondari Gerezani, Ilala, Dar es Salaam,  wao wanasema hawana kazi ndogo. Wanadai ndio wababe wa tuzo, na wako...
14/11/2024

Shule ya Sekondari Gerezani, Ilala, Dar es Salaam, wao wanasema hawana kazi ndogo.

Wanadai ndio wababe wa tuzo, na wako tayari kwa hilo. Wakiwa ndani ya MODOLO Creative Media chini ya EConnect, tayari wamemaliza yao, wanasubiria siku ya tukio.

Je, hii ni kweli?

Ni katika 07/12/2024 tunaenda kushuhudia mapinduzi katika tasnia ya sanaa pale Msasani Beach Club.

Kwa swali au maoni au kudhamini piga simu 0769409240/0788741194

tanzania




@





Wakati tunaelekea kwenye tamasha letu kubwa la ,  tusisahau kuwa kuku aina ya Horasi ndiye kuku wa asili anayeshika namb...
14/03/2024

Wakati tunaelekea kwenye tamasha letu kubwa la , tusisahau kuwa kuku aina ya Horasi ndiye kuku wa asili anayeshika namba moja kwa ubora pamoja na soko, si tu Tanzania bali hata soko la Kimataifa.

Unaweza kuanza kidogo, na kufikia pakubwa.

Tukutane 27/04/2024 ili kuona makubwa yaliyopo kwenye tasnia ya ndege wafugwao hususani kuku.

Wanafunzi wote na walimu watahamia uwanja wa Mnazi Mmoja kula kuku, kuburudika na burudani na kufurahi.

Hakikisha k**a una shule yako, isikose kushiriki.

Kwa maswali au maoni usikose kupiga simu 0769409240/0758061582




Unaweza kuweka nafasi kwa ajili ya kuhudumia siku ya Tamasha letu la Kujisajili tuma meseji whatsapp kupitia 0769409240.
18/02/2024

Unaweza kuweka nafasi kwa ajili ya kuhudumia siku ya Tamasha letu la

Kujisajili tuma meseji whatsapp kupitia 0769409240.

Wakati Mheshimiwa Rais  amefungua fursa za utalii nchini, eneo mojawapo lenye fursa kubwa ya kuchangamkia ni kuku wa asi...
26/01/2024

Wakati Mheshimiwa Rais amefungua fursa za utalii nchini, eneo mojawapo lenye fursa kubwa ya kuchangamkia ni kuku wa asili.

Kuku wetu wa asili anautangaza utamaduni wa Kitanzania. Kila mgeni anayeingia nchini, bila shaka kuku wa asili atakuwa ni moja ya kitoweo cha kumkaribisha.

Ladha nzuri ya kuku wetu wa asili na ubora wake, ni kitu pekee kinachoweza kufungua na kukuza masoko ya kuku wa asili kimataifa.

Ndio maana tunapomzungumzia kuku wa Horasi, tayari tunamuweka kuku huyu kwenye sura ya kushindana na soko la Kimataifa na kuingiza fedha nyingi kwa nchi yetu.

Wakati inaonesha ifikapo 2030 tutakuwa na uhaba mkubwa wa nyama ya ng'ombe na mbuzi kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa yanayoathiri malisho, sehemu pekee itakayotegemewa kwa sana kutoa nyama ni kwenye sekta ya kuku.

Hii inatuonesha kwamba inatakiwa tujiandae, na kuandaa vijana waione fursa na kuanza kuchangamkia mapema.

Ndio sababu kubwa ya miongoni mwa malengo yake kwa wanafunzi ni kutoa fursa ya mafunzo ya stadi za maisha na ujasiriamali katika tasnia ya kuku wa asili ili kuhakikisha wanafunzi wanaanza kujiandaa mapema katika ushindani huo.

Sababu kubwa ya kuku wa asili mbali na kutangaza utamaduni wa kitanzania, ila kuku huyu anafugika kwa gharama ndogo sana na ana uwezo wa kuzaliana. Hivyo anatoa fursa kwa vijana au wanafunzi kutumia muda wa ziada katika kufuga ili kujiongezea kipato na kukabiliana na changamoto za lishe duni na ajira.

Kuku wa asili anafugika vizuri kibiashara, na anakua kwa wakati endapo tu utakuwa na mbegu bora na elimu ya kutosha katika ufugaji.



.

Milango ya udhamini imefunguliwa tayari, kuwasiliana nasi piga simu 0769409240/0758061582.



















m





tz

Horasi ni kuku wa asili ya Kitanzania ambaye chimbuko lake ni kanda ya ziwa.Kuku wa Horasi ana umbo kubwa na huwa na uwe...
25/01/2024

Horasi ni kuku wa asili ya Kitanzania ambaye chimbuko lake ni kanda ya ziwa.

Kuku wa Horasi ana umbo kubwa na huwa na uwezo wa kufikia 3Kg hadi 4Kg ndani ya miezi 5 kwa jogoo na 2Kg hadi 3Kg tetea.

Kuku huyu ana sifa ya kuatamia mayai mengi kati 12 hadi 18 kwa wakati mmoja na kuyatotoa yote.

Wakati wa ukuaji wake vifaranga wanakua na manyoya machache sana, wanakuwa warefu sana.

Kuku wa asili aina ya Horasi, ni kuku anayejitambulisha yeye mwenyewe bila mfugaji kutumia nguvu kumnadi.

Kuku huyu amekuwa na soko kubwa ndani na nje ya nchi ya Tanzania.

Kutokana na ukubwa na uzito wake anaofikia akiwa bado ana umri mdogo, inamfanya kuku huyu wa Horasi kuwa na sifa ya kushindana soko la kimataifa.

Uzito wa kuku anaoupata wakati akiwa na umri mdogo, unamfanya awe na vigezo bora kidunia (Global Standards) hivyo kutoa muelekeo mzuri kwa kuku wa Kitanzania ambaye tuna uwezo wa kumnadi kibiashara.

Wakati wa tutakula kuku wa asili tu, tutaweza kumwelewa vizuri kuku huyu kuanzia ubora na utamu wake, na jinsi ya kumfuga kibiashara.



.

Milango ya udhamini imefunguliwa tayari, kuwasiliana nasi piga simu 0769409240/0758061582.


















m





tz

Wakali wa mapishi na ubunifu wa bidhaa zitokanazo na mazao ya kuku wanaenda kufanya yao. Si wengine, bali wanafunzi ndan...
24/01/2024

Wakali wa mapishi na ubunifu wa bidhaa zitokanazo na mazao ya kuku wanaenda kufanya yao.

Si wengine, bali wanafunzi ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam wakichuana kutoka kila Wilaya ili tumpate mbunifu bora wa bidhaa za mazao ya kuku.

Je, shule yako tayari imefikiwa ili kushiriki ?

K**a bado, basi usibaki nyuma, hakikisha wanafunzi wako wanashiriki kuonesha makali yao.

Wasiliana nasi kupitia 0769409240/0758061582 ili kushiriki kwenye mashindano na TUZO hizi.



.


















m





tz

Karibu Mgeni wetu Rasmi Katibu Mkuu, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.Tunatambua kuwa utamaduni ni kitambulisho cha...
23/01/2024

Karibu Mgeni wetu Rasmi

Katibu Mkuu, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Tunatambua kuwa utamaduni ni kitambulisho cha jamii husika kupitia mambo mbalimbali mfano chakula, mavazi, lugha n.k.

Tanzania yapo mambo mbalimbali yanayotutambulisha utamaduni wetu k**a lugha yetu adhimu ya Kiswahili na vyakula vyetu mfano Kuku wa Asili.

Kwa sasa kuku wetu wa asili anaelekea kupotea nchini na tunaona wazi kwamba wale walaji wakubwa wa kuku huyu wanapata tabu katika kupatikana kwake hasa kuku asili halisi.

Kupitia tunaenda kumrudisha kuku huyu wa kututambulisha si tu kwa sababu ya utamu wake, bali kupitia faida zake nyingi za kiafya mwilini mwetu na kiuchumi.

Tamasha letu hili, litaenda kuhamasisha wanafunzi na jamii kwa ujumla juu ya kupenda kula mazao ya kuku wa asili kwa kuzingatia afya bora, pamoja na kuhakikisha kila familia ihakikishe inamfuga kuku huyu wa asili kuendeleza uwepo wake.

Wanafunzi watapata stadi za maisha na ujasiriamali kuweza kuelewa na kujua jinsi ya kumtunza kuku wa asili ili asipotee pamoja na faida zake kiafya na kiuchumi.

Tutambue ni kuku wa asili pekee ndiye mwenye kuitambulisha Tanzania nje ya nchi na kuwavutia wageni hasa watalii kumtumia na kufuraia kuku halisi wa Kitanzania, pamoja na kuwa sehemu ya kukuza pato la Taifa kupitia sekta ya Utalii.

.

Milango ya udhamini imefunguliwa tayari, kuwasiliana nasi piga simu 0769409240/0758061582.


















m





tz






Kuku ni Uchumi | Kuku ni Lishe | Kuku ni Ajira.             m       tz
22/01/2024

Kuku ni Uchumi | Kuku ni Lishe | Kuku ni Ajira.



















m





tz

21/01/2024

Kuku ni suluhisho katika kukabiliana na udumavu kwa watoto.
21/01/2024

Kuku ni suluhisho katika kukabiliana na udumavu kwa watoto.



Ni tukio la kihistoria, kwa shule zote za Mkoa wa Dar es Salaam kuchuana katika kutafuta Tuzo kwenye ubunifu wa bidhaa z...
20/01/2024

Ni tukio la kihistoria, kwa shule zote za Mkoa wa Dar es Salaam kuchuana katika kutafuta Tuzo kwenye ubunifu wa bidhaa zinazokana na mazao ya kuku.

Tasnia ya kuku inafungua fursa, inakuza uchumi na kuondoa changamoto ya udumavu.

Tutachoma kuku, Tutakula kuku.

Tutapika mayai, Tutakula mayai.

Tutaona bidhaa za mazao ya kuku, Tutakula bidhaa za mazao ya kuku.

.
.

Tayari tumefungua milango kwa wadhamini, wasiliana nasi kwa maelezo zaidi kupitia 0769409240/0758061582


















m





tz

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255758061582

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when School KukuChoma Carnival posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

  • Want your business to be the top-listed Event/venue?

Share