14/09/2026
Takriban waendesha pikipiki 100 walikusanyika nje ya Msikiti wa Kaunas nchini Lithuania wakati Waislamu wakiendelea na Swala ya Ijumaa.
Waendesha pikipiki hao walivurumisha injini, kupiga muziki kwa sauti kubwa, kupiga kelele na kuwarekodi waumini waliokuwa katika ibada.
Inadaiwa pia kuwa kundi hilo lilifika na kichwa cha nguruwe na kuwaonyesha waumini waliokuwa wakiendelea na ibada katika eneo la msikiti, jambo ambalo jamii ya Waislamu imelielezea k**a kitendo cha makusudi cha kuwatisha na kuwafedhehesha waumini wakati wa ibada.
Pamoja na usumbufu huo, waumini walibaki watulivu na waliendelea na Swala yao hadi mwisho.
Polisi nchini Lithuania wameanzisha uchunguzi wa kiutawala ili kubaini iwapo tukio hilo linaweza kuhusisha uchochezi au vitendo vinavyolenga kundi fulani la watu.
Jamii ya Waislamu ya Kaunas imelaani tukio hilo na kusisitiza kuwa uhuru wa dini unapaswa kumruhusu kila mtu kuabudu kwa amani, usalama na bila vitisho.
Una maoni gani kuhusu tukio hili?