22/09/2022
UKWELI ULIVYO
Juma Mgunda katika njia za Pitso Mosimane
Imekuwa ni desturi yetu sisi watanzania kubeza watu wetu kwa kuona hawana ubora, lakini tupo tayari kuimba majina ya wageni hata k**a uwezo wao ni wa kawaida kabisa katika soka letu kwakuwa tu bado tunaandamwa na jinamizi la kasumba ya kuamini mgeni pekee ndio anaweza kufanya mambo makubwa katika soka letu (ni utumwa wa kifikra tu) hususa ni katika hizi timu kubwa jambo ambalo linazika vipaji vingi na uwezo wa wazawa wengi katika soka letu.
Ipo hivi, tunalalamika sana kwamba hatuna makocha wengi wazawa lakini ukweli ni kwamba uhaba wa makocha wazawa unachagizwa na dhihak, kejeli na dharau kwa mashabiki na baadhi ya wadau wa soka
Kivipi, lilipoibuka suala la JUMA MGUNDA kuhusishwa na klabu ya SIMBA hii ilikuwa ni neema kubwa sana katika soka letu la Tanzania lakini kwa bahati mbaya bila ya tafiti za kina baadhi ya wadau na mashabiki walikuwa mstari wa mbele kukosoa kwamba Mgunda hastahili kuwa kucha wa Simba wa muda wakiamini kwamba haendani nayo na wengine walidai hana vyeti, na wengine waliamini Simba ndio mwisho wao hatua za awali kwakuwa katika benchi kwenye mechi ya mashindano ya CAF imeongozwa na Mtanzania.
Ukweli ulivyo, Uwepo wa Mgunda pale Simba ni tiba kubwa katika fikra za wadau wengi wa soka ambao wanaamini katika wageni na hata wageni wanaposhindwa kufanya vizuri basi wanaamini wazawa wana msaada tu wakati wa matatizo (migogoro)tu lakini katika kipindi cha neema klabuni basi wageni ndio wapewe timu.
Juma Mgunda katika njia za Pitso Mosimane naamini k**a Simba watamuamini Mgunda na kumuachia timu k**a kocha wa kudumu Mgunda atakwenda kuwa kocha mkubwa barani Afrika k**a ilivyokuwa kwa Pitso Mosimane na hata Ibenge, pale Simba pana kila aina ya facilities zitakazo msaidia Mgunda k**a Kocha mkuu kwani wachezaji wa kushindana CAF wapo na timu inajimudu hivyo kwake itakuwa ni rahisi sana kuonesha kile kitu alichonacho kutokana na taaluma yake ya ukocha. Naamini Mgunda ni Pitso wa Tanzania kwani ameshaweza kuprove mambo mengi sana kwa ligi ya ndani na ameweza kusumbua vichwa makocha wa timu kubwa hapa nchini kwa kuwafunga na hata kutoa sare.
K**a Simba wataendelea kumuamini na timu ikafanya vizuri katika mashindano haya ya klabu bingwa naamini JUMA MGUNDA anakwenda kutambulika Afrika kwa haraka sana kwanza kupitia bland ya timu anayoifundisha katika soka la Afrika inafatiliwa sana kwasasa hivyo sitoshangaa kumuona klabu kubwa katika maeneo mengine ya Afrika baada ya kuondoka Simba hapo baadae. Ikumbukwe hata Pitso Mosimane amekuwa kocha mkubwa Barani Afrika baada ya kuaminika na klabu kubwa nchini kwao ya Mamelod hvyo hata njia hii ya Mgunda ni k**a njia ile ya Pitso Mosimane.
Karibu, follow, share, like na comment kwa taarifa za ukweli na uhakika
Enjoy soccer na Mayagillah sports fact