07/05/2026
Mahaba yana pofusha wengi!
Au Ubaguzi unasahaulisha wengi!
Kuna mtu mahali amezoea kupita na kila aina ubaya kwa wengine bila kujulikana, ila siku ambayo mambo yamegeuka hutafuta huruma kwa wasiokuwepo au wasiojua mwanzo wa mambo k**a wapambe wake.
Mfano umetendwa jambo k**a miaka 30, au 20, au 10 iliyopita, wewe mwenzangu ambaye haukuwepo katika picha unanoa mdomo ili iweje, kwamba unajua kuzungumza sana au..?
Kuna watu ni mashetani sirini, ila kwenye macho ya wengi ni watakatifu, ninapowafungia nje ya maisha yangu, uliza kwanza kabla ya kuanza kunoa mdomo.
Fikiri kabla ya kutenda au tafakari Kila mara kabla ya kurukia vitu. Tuchukulie mfano, haujawahi kuonekana umuhimu wa kuunganisha watu k**a familia, badala yake juhudi zilifanyika za kuhakikisha hakuna maelewano, kujenga umoja na wala kuheshimu chaguzi za wenzako. Leo unapata nguvu wapi ya kuamini yale uliyoyapiga vita ni sehemu ya maisha yako sasa?
Mfano mwingine, una Mtoto ambaye alifika nyumbani kwako mara mbili tu katika maisha yake, akiwa na miaka miwili na nusu (hakukubalika) na hakuna aliyemfuatilia baada ya hapo, hadi alipofika miaka 21 kwa mashinikizo ilitakikana aje, kwakuwa sasa tumetaka sisi na baba yake ana kazi, ila mama alipokuwa na kazi na alipojaribu kumleta, mlihakikisha hawaelewani na tunamzuia aje kwa kuwa siyo nyie mmetaka, na hata akija atakwenda kwa wazazi wa mama. Bila kujali maumivu ya Mtoto, ubabe ulifanyika akarudia njiani.
Kweli kwa mara ya pili alifika kunakodhaniwa ni kwao akiwa mtu mzima kwa mashinikizo na ubabe. Ila kwa kifupi, mara ya tatu angekuja katika mazingira ya majonzi tena kwa heka heka za wasiojua mbele wala nyuma, NAMI NIMEKATAA.
K**a hakuna kuheshimu nafasi za wazazi waliopambana kwa miaka zaidi ya 30 ya uvunjanji wa haki ya Kila mtu kujichagulia ampendaye basi na asije. Haukuwepo kwenye maisha yetu, lipi unalojua anyway, zaidi ya kukaa kimya? Ulifanya nini wakati ilipotakiwa jambo lifanyike ili kunusuru utengano wa muda mrefu na mwanafamilia mwenzenu?